Skip to main content

MTOTO ALIYEIBWA HOSPITALI AKIWA NA SIKU 19 MWAKA 1987, AUNGANA NA WAZAZI WAKE BAADA YA MIAKA 21.





Carlina  White



 
Carlina  White  na  wazazi  wake  halisi.


Tarehe  18 Agosti  1987 ilikuwa  ni  siku  mbaya  kabisa  kuwahi  kutokea  katika  familia  ya  Bi Joy  White  na  Carl  Tyson.


Carlina   White  na  mama  yake  mzazi.

Mtoto  wao  kipenzi  aliyekuwa  na  siku kumi  na  tisa  tu  tangu  aanze  kuvuta  pumzi  alitekwa  katika  hospitali  ya  Harlem Hospital  Center, New  York  City, Marekani.

 
Carlina  White  mwaka  1987  kabla  hajatekwa. 

 
Wazazi wa  Carlina  mwaka  1987

Wazazi  wa  Carlina  mwaka  1987

Hata  hivyo, miaka  ishirini  na  moja  baadaye  mtoto  huyo  alikuwa  na  re united  na  wazazi  wake  katika  namna  iliyo  staajabisha  kabisa.
Ilikuwaje  ?


 
Ann Petway, mwanamke  aliyemteka  Carlina  mwaka  1987.

Fuatana  name  katika  simulizi  hii  ya  kusisimua.
Tarehe  15  Julai  1987  ilikuwa  siku  ya  furaha sana  kwa wanandoa   Joy  White  na mume  wake  Carl  Tyson kwa  sababu  ilikuwa  ni  siku  waliyo  barikiwa  kupata  mtoto  wao  wa  kwanza. ( Ndoa  ilikuwa  imejibu )

Kwa furaha  aliyokuwa  nayo, baba  wa  mtoto  alimpa  mtoto  wake  jina  linalo  fanana  na  lake. Baba  aliitwa Carl, so  mtoto  akamuita  Carlina. Kama  angekuwa  anaitwa  Joseph  basi  bila  shaka  angemuita  Josephina.

Mtoto  alizaliwa  salama na baada  ya  masaa  24  tangu  ajifungue  mzazi aliruhusiwa  kurudi  nyumbani. Lakini  siku  moja  tangu  waruhusiwe  kurudi  nyumbani, mtoto  alianza  kulia  kwa  nguvu  bila  kukoma jambo  lililo wafanya wazazi  wake  wamrejeshe  hospitalini  hapo  haraka  sana, ambapo  alifanyiwa  vipimo.

Ilionekana kuwa  mtoto  Carlina  alimeza  maji  maji  wakati  wa  kujifungua  na  kupata  maambukizi. So  mama  pamoja  na  mtoto  wake  wakalazwa  kwa  matibabu  ya  mtoto.

Siku  mbili  baadaye  mwanamke  mmoja  kwa  jina  Annugetta  “ Ann” Pettway  alianza  kuzoeana  na  mama  Carlina. Ann  alijifanya  ni  nurse   lakini  haja ajiriwa  katika  hospitali  hiyo, ila yupo  hapo  kwa  shughuli  ambazo  mama  Carlina  hakuzielewa.

Ann  aliendelea  kuonekana  katika  hospitali  hiyo kwa  wiki  tatu  mfululizo na  katika  kipindi  hicho  cha  wiki  tatu  alifanikiwa  kumshawishi  mama  Carlina  kiasi cha  kumfanya  amuamini.
Siku  moja  mama  Carlina  alipata  udhuru  na  kumuomba  Ann amsaidie  kumuangalia  mtoto  wake (  Carlina ).  Hilo  lilikuwa  ni  kosa  kubwa sana  katika  maisha  yake.
Alfajiri  ya  siku  hiyo  majira  ya  saa  nane, wakati  wa  kubadilishana  shift  kwa  wafanyakazi, Ann  alifanikiwa  kutoroka  na  mtoto  Carlina.
Kulikuwa  na  Video  Surveilance  lakini  wakati  Ann  anatoroka  na  Carlina  zilikuwa  hazifanyi kazi.  Hakukuwa  na  picha  yoyote  ya  Ann  wala  hakukuwa  na  namna  yoyote  wangeweza  kujua  sura  ya  Ann isipokuwa  kwa  maelezo  waliyo  pewa  na  Joy  White  na  Carl  Tyson, ambao  ni wazazi  wa  Carlina.
Ilipofika  saa  mbili  za  asubuhi, uongozi  wa Harlem  Hospital  Center  aligundua  kukosekana  kwa  mtoto  Carlina.
Muda  mchache  baadaye, habari  ziliwafikia  wazazi  wa  Carlina, ambao   walipanic  na  kwenda  hospitalini  hapo  only  to prove  that  their  lovely  baby  was  missing.
NYPD  walitangaza   kupotea  kwa  mtoto, na  kuahidi  zawadi  ya  dola  elfu  kumi  kwa  mtu  atakaye  fanikisha  kupatikana  kwa  mtoto  Carlina.
Picha  ya  mtoto  Carlina  pamoja  na  picha  ya  kubuni  na  Ann  zilisambazwa  nchi  nzima  lakini  hata  hivyo  hazikuzaa  matunda.
Mwaka  1989  wazazi  wa Carlina  walifungua  kesi  ya  madai  ya  ya  fidia  ya  Dola  Milioni  Mia  Moja  dhidi  ya Harlem Hospital   Centre  na  mwaka  1992  mahakama  iliamua  walipwe   DOLA  LAKI  SABA  NA  NUSU ambazo  walilipwa  mwaka  huo  huo.
BAADA   YA  KUMTEKA  CARLINA.
Baada  ya  kumteka  Carlina , Ann  alipanda  treni  na  kuelekea  kwenye  jiji  la   Bridgeport, Connecticut, kilo  mita  chache  kutoka  New  York.
BAADA    YA   KUFIKA   CONECTICUT.
Baada  ya  kufika  Connecticut, Ann  alimlea Carlina  kama  mtoto  wake  wa  kumzaa.  Kabla  ya  yote  alimbadilisha  jina  na  kumuita  Nejdra  “ Netty” Nance.
Mwaka  1993, ikiwa  ni  miaka nane  tangu  amteke  mtoto  Carlina, Ann    alihamia  Atlanta  na  kuendelea  na  maisha  yake  kama  kawaida.

CARLINA  AANZA  KUMTILIA  SHAKA  ANN.
Akiwa  na  umri  wa  miaka  23, Carlina  alianza  kumtilia  shaka  Ann  kama  ni  mama  yake  mzazi  kweli.  Sababu  zilizo  mfanya  awe  na  mashaka  ni  kwanza; kutokuwa  na  ufanano  wowote  kati  yake  na  mama  yake, lakini  pili   ni  kutokuwepo  na  nyaraka  muhimu  zinazo  thibitisha  kama  Ann  ni  mama  yake  kweli,  kama  vile  cheti  cha  kuzaliwa  na   Social  Security  Card.
Siku moja, Carlina  alikuwa  na  issue  ambayo  ilimhitaji  apelike  cheti  chake  cha  kuzaliwa  ambapo  alimfuta  Ann  na  kumtaka  ampe  cheti  hicho,  Ann alitoa  cheti  cha  kughushi  na  Carlina  alipokipeleka  kilichunguzwa  kwenye  data  base  na  kuonekana  kuwa    hakuna  mtoto  aliyezaliwa  mwaka 1987  mwenye  jina  lake  ( Nejdra  Nance ), si  Atlanta  wala  si  Connecticut.

Carlina  alirejea  kwa  mama  yake  wa kughushi ( Ann ) akiwa  ame fyumu  na  kumtaka  amuonyeshe  cheti  chake  cha  kuzaliwa.
Ann  akaamua  kumwambia  ukweli  kuwa, yeye  ( Ann ) si  mama  yake  mzazi, akamdanganya  kuwa  mama  mzazi  wa Carlina alikuwa  muathirika  wa  dawa  za  kulevya,na  alimuachia  yeye  ( Carlina ) amtunze bila  kumpa  documents  zake  muhimu  kama  cheti cha  kuzaliwa nakadhalika.
UAMUZI   WA   CARLINA :
Carlina  alianza  kufanya  upelelezi  wake  binafsi, ambapo  kwa  msaada  mkubwa  sana  wa  kituo  cha  National  Center for  Missing  and  Exploited  Children alifanikiwa  kuunganishwa  na  wazazi wake.
Ann  Pettway  alikamatwa, kushitakiwa  na  kufungwa  miaka  kumi  na  mbili, kifungo  anacho  kitumikia  tangu  mwaka  2010.

KITU  GANI  KILIMFANYA  ANN  ACHUKUE  UAMUZI  WA  KUMTEKA  MTOTO  MCHANGA  NA  KUMLEA  KAMA  MTOTO  WAKE.
Tatizo  lililo  mfanya  Ann  amteke  mtoto  mchanga  ni  kuchoropoka  kwa   mimba ( miscarriage )
Ilifahamika  kuwa, Ann   kabla  hajafikia  uamuzi  wa  kumteka  Carlina  alibeba  mimba   nne  na  zote  zilikuwa zikichoropoka.
Mwezi  huo  huo  wa  saba  1987 Ann  alijifungua (mimba yake ya  nne  )  lakini  mtoto  alikufa  wakati  wa  kujifungua.
Ann  alikata  tama  ya  kuzaa  mtoto  na  kutaka  kurudi  nyumbani  kwao  na  hadhithi  ile  ile  iliyozoeleka, kwamba ujauzito  umeharibika, alicho  kifanya  ni  kwenda  kwenye  hospitali  ya  mji  mwingine, kuiba  mtoto  na  kurejea  nae  nyumbani  kwao  akijifanya  kuwa  ni  mtoto  wake  wa  kumzaa.
Ndugu  zake  hawakuwa  na  mashaka  yoyote  na  mtoto  huyo kwa  sababu  Ann aliondoka  nyumbani  kwao  na  ujauzito  wa  miezi  tisa   akiwa  anaelekea  hospitali  kujifungua.
TUKIO  HILI  LA  KUSISIMUA  LIMETENGENEZEWA  FILAMU   INAYO  ITWA : ABDUCTED :  THE  CARLINA  WHITE  STORY.
Unaweza  kuitafuta  kwenye  maduka  mbalimbali  ya  filamu  au  kwenye  internet

Mahojiano  kati ya  Carlina  White  na  vyombo vya  habari  baada  ya  kuwa  reunited  na  wazazi  wake , unaweza  kuya  cheki  hapa:


KAMA  NA WEWE  UNAYE  SOMA  HABARI  HII, UNA  TATIZO  LA  KUCHOROPOKA  KWA  MIMBA, TEMBELEA  http://neemaherbalist.blogspot.com/2013/12/dawa-asilia-ya-kuzuia-kuchoropoka-kwa.html

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA