Skip to main content

TUMIA KAROTI KUJI KINGA DHIDI YA SARATANI UGONJWA WA MOYO





 KATIKA  makala  yaliyopita  tuliangalia  faida  za  karoti  kwa  afya  ya  mwili  wa  mwanadamu, leo  tunaangalia  namna  tunavyoweza  kutumia  karoti  kama  kinga  ya  ugonjwa  wa  saratani  na  magonjwa  ya  moyo..ENDELEA. 

Kama karoti imestawishwa kwa kutumia madawa ya mimea na mbolea au kama huna uhakika na usafi wake, ni vizuri ukwangue maganda yake ya juu na kuyaondoa. Unaweza kuamua kukata vipande virefu au vya mviringo, kukata na mashine maalum vipande vidogo vidogo au kula nzima nzima.

Karoti ni tamu vyovyote utakavyoamua kuila, iwe mbichi au iliyochemshwa. Ingawa kula karoti mbichi ni bora zaidi, lakini hata ukila iliyopikwa bado haipotezi virutubisho vyake, zaidi inaelezwa kuwa, kambalishe, virutubisho pamoja na sukari yake inapatikana kirahisi na hivyo kuifanya kuwa tamu.

Jambo la kuzingatia kama ukiamua kuipika, usiipike sana, bali inatakiwa kuchemshwa au kupikwa kwa muda mfupi ili virutubisho vyake visipungue au kupotea kabisa.

DONDOO ZA KUTENGENEZA KAROTI
Unaweza kuitengeneza karoti kama unavyotaka ili kupata ladha tofauti bila kupoteza virutubisho vyake. Unaweza, kwa mfano, kutengeneza saladi ya karoti kwa kuchanganya na majani yake kwa kukatakata vipande.

Aidha, unaweza kutengeneza saladi kwa kukata vipande vidogo vidogo kisha kuchanganya tufaha na matango na kula pamoja kwenye mlo wako wa siku kama kachumbari.

Unaweza kutengeneza supu ya karoti kwa kuchemsha vipande vyake na nyanya. Chukua karoti na nyanya ulizochemsha, kisha weka kwenye ‘blender’ au chombo kingine unachoweza kusagia. Saga mchanganyiko huo ili kupata supu, unaweza kuongeza viungo vingine ili kupata ladha. Unaweza pia kuinywa ikiwa ya moto au ikiwa imepoa.

Kinywaji kingine unachoweza kutengeneza kwa afya yako ni juisi ya karoti, ‘soymilk’ na ndizi mbivu. Tengeneza nusu glasi ya juisi ya karoti, chukua glasi moja ya soymilk na ndizi mbivu moja kisha changanya kwa kutumia ‘blender’. Kama huna changanya kwa kutumia kijiko au mwiko na kupata ‘milk shake’ ya ukweli.

KAROTI IKIZIDI MWILINI
Ingawa siyo rahisi kutokea lakini inawezekana kuna watu matumizi ya mboga hii kwao yako juu. Karoti ikizidi mwilini, huweza kumfanya mtu aonekane ‘wa njano’, hasa katika sehemu za viganja vya mikono, nyayo za miguu na nyuma ya masikio. Kitaalamu hali hii hujulikana kama ‘carotoderma’.

Hata hivyo, hali hiyo hutoweka pale mtu huyo anapopunguza ulaji wa karoti au vyakula vingine vyenye kiwango kikubwa cha virutubisho vya ‘carotene’ na hakuna madhara mengine anayoweza kuyapata.
Mwisho, katika nchi za Asia, ambako ndiko karoti inaelezwa kuanzia, inaaminika pia kuwa na uwezo wa kurekebisha masuala ya nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya kufanya mapenzi (sexual dysfunction & sexual drive).

Pia karoti inaaminika kuimarisha ufanisi wa figo na kuondoa hewa chafu na baridi mwilini. Baada ya kujua faida za karoti, bila shaka kuanzia leo umepata sababu ya kuiangalia upya karoti kama ‘mzizi’ muhimu kwa afya yako.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA