Skip to main content

Ushauri wa chakula na lishe wa jinsi ya kukabiliana na matatizo ya kiafya yanayoambatana na kuwa na saratani au tiba yake:



                             
Matumizi  Ya  Sigara  Kwa  Muda  mrefu  huweza  kusababisha  kansa.
                                      Ugonjwa wa  saratani
Saratani ni ugonjwa unaotokana na seli za mwili zilizopoteza mfumo wake wa kugawanyika na hivyo hazipo katika hali yake ya kawaida. Seli huweza kugawanyika bila mpangilio maalum na kuharibu mkusanyiko wa seli nyingine. Seli za saratani hutokea sehemu moja ya mwili na zinaweza kusambaa sehemu nyingine za mwili, saratani pia husababishwa na hali ya mazingira ya vitu mbalimbali kama vile ulaji wa vyakula vyenye visabbishi vya saratani (carcinogenic compounds), ulaji usiofaa, unywaji 12
wa pombe, uvutaji sigara au minoni hatari, “asbestos” lisasi (lead), uranium na zebaki.
Zipo pia baadhi ya saratani zinazosabishwa na virusi kama hepatitis B ambayo huleta saratani ya ini na human papiloma inahusishwa na saratani ya shingo ya kizazi. Saratani huweza kutokea kwenye sehemu mbalimbali za mwili kama vile mapafu, matiti ovary, kibofu cha mkojo, shingo ya uzazi, utumbo, koo, kinywa, tezi dume (prostate), ini na ngozi.
Ulaji unaofaa na mtindo bora wa maisha ni vigezo muhimu sana katika kuzuia saratani na pia ni sehemu muhimu ya matibabu na kudumisha maisha bora baada ya kupata matibabu. Matumizi ya baadhi ya vyakula huweza kuongeza uwezekano wa kupata saratani. Uzito wa mwili ukiwa mkubwa unaweza pia kuongeza uwezekano wa kupata baadhi ya saratani Ni muhimu kufuata mtindo bora wa maisha kwani ni bora kuzuia kuliko kutibu.

Mambo yanayohusiana na mtindo wa maisha yanayoweza kuchangia katika kupata saratani.

Tafiti zinaonesha kwamba saratani za kurithi ni chache sana ila saratani nyingi hutokana na sababu za kimazingira. Tafiti nyingi zimeonesha kuwa kiasi cha asilimia 40 hadi 60 za saratani husababishwa na mtindo wa maisha usiofaa hasa ulaji usiofaa na kutofanya mazoezi ya mwili. Mtindo wa maisha usiofaa unajumuisha:
 Ulaji wa vyakula vyenye nishati-lishe kwa wingi ambavyo husababisha unene. Unene umeonekana kuhusiana na saratani ya mji wa uzazi, matiti, figo, tezi dume, utumbo mpana na kibofu cha mkojo;
 Ulaji wa nyama nyekundu kwa wingi na zile zilizosindikwa vimehusishwa na saratani ya tezi la kiume, utumbo mpana, mapafu, kinywa na koo;
 Utumiaji wa pombe kwa wingi huongeza hatari ya kupata saratani ya mdomo, koo, koromeo, utumbo mpana, kongosho, ini na matiti;

Ushauri wa chakula na lishe wa jinsi ya kukabiliana na matatizo ya kiafya yanayoambatana na kuwa na saratani au tiba yake:

Matatizo mbalimbali yanaweza kujitokeza kutokana na hatua ya ugonjwa au aina ya matibabu mgonjwa anayopata, hasa dawa za saratani (chemotherapy) au mionzi. Matatizo hayo ni kama kukonda, upungufu wa 
damu, kukosa hamu ya kula, kichefuchefu, kutapika, kuhara, kukosa choo, vidonda kinywani, na matatizo ya ngozi.

Kukonda
Wagonjwa wengi wa saratani wanapungua uzito wakati wa matibabu. Hii inaweza kusababishwa na madhara ya saratani yenyewe, ongezeko la mahitaji ya virutubishi mwilini, kukosa hamu ya kula, aina ya matibabu anayopata mgonjwa (dawa, mionzi au upasuaji). Yafuatayo huweza kusaidia katika kukabiliana na tatizo hili:
 Kuzingatia ulaji wa mlo kamili na ulaji wa aina mbalimbali za vyakula;
 Kuongeza ulaji wa vyakula vyenye protini kwa wingi yenye asili ya wanyama (isipokuwa nyama nyekundu) na mimea.
 Kula vyakula vilivyo laini vilivyoboreshwa na kuongezewa vyakula vyenye protini na nishati-lishe kwa wingi.
 Kula milo midogo midogo mara kwa mara na kuongeza asusa zenye virutubishi vingi;
 Kujitahidi kula wakati una hamu yakula au ukiwa na njaa kali na kula vyakula vile vyenye virutubishi kwa wingi;
 Kufanya mazoezi kabla ya kula (kama vile kutembea) ili kuongeza hamu ya kula na kusaidia uyeyushwaji wa chakula;
 Kula taratibu, usile kwa haraka bali jipe muda wa kutosha wakati wa kula;
 Kutumia viungo vyenye harufu unayoipenda
 Kutumia vinywaji kati yam lo na mlo na sio wakati wa kula kuepuka tumbo kujaa na hivyo kushindwa kula chakula cha kutosha; na
 Kutumia vinywaji vyenye virutubishi vingi na nishati-lishe.


Upungufu wa wekundu wa damu

Upungufu wa wekundu wa damu huweza kusababishwa na saratani yenyewe au matibabu yake. Pia huweza kutokana na ulaji duni hususani kula vyakula vyenye upungufu wa madini chuma; malaria au minyoo.
Upungufu wa wekundu wa damu huweza kukabiliwa kwa:-
Kula vyakula vyenye madini chuma kwa wingi hususan vyenye asili ya wanyama (epuka nyama nyekundu). Aina ya madini chuma iliyopo katika mayai na maziwa haifyonzwi na mwili kwa ufanisi. 14

Kula matunda kwa wingi kila siku. Tumia matunda kwa wingi kila siku. Tumia matunda yenye Vitamini C kwa wingi pamoja na mlo kwani husaidia ufyonzwaji wa madni chuma yanayopatikana kwenye vyakula vya mimea.
 Kuepuka vinywaji vyenye kafeini kama chai, kahawa au soda wakati wa mlo kwani huzuia ufyonzwaji wa madini chuma yanayopatikana kwenye vyakula vya mimea;
 Kutumia vinywaji kama togwa, rozela, mtindi au uji wa kimea kwan vinaongeza ufyonzwaji wa virutibishi muhimu; na
 Kufuata ushauri wa mtaalam wa afya kuhusu matumizi ya vidonge vya madini chuma na foliki aside na kutibiwa magonjwa kama vile malaria na minyoo.

Kukosa hamu ya kula

Kukosa hamu ya kula ni moja ya matatizo yanayoweza kusababishwa na saratani yenyewe au matibabu yake. Yafuatayo yanaweza kuongeza hamu ya kula:
 Kujaribu vyakula vya majimaji au vilivyopondwa;
 Kula milo midogo midogo mara nyingi kwa siku badala ya kula chakula kingi kwa mara moja;
 Kutumia vyakula vyenye nishati-lishe kwa wingi;
 Kuongeza asusa na kuziweka sehemu ambayo ni rahisi kuchukua mtu anaposikia hamu;
 Kunywa vinywaji mbalimbali kama juisi halisi ya matunda, supu na vinginevyo, kidogo kidogo mara kwa mara;
 Kufanya mazoezi ya mwili kwani husaidia kuongeza hamu yakula
 Kutumia viungo kwa kiasi katika chakula;
 Kujaribu kubadili aina na ladha ya vyakula unavyotumia; na
 Kula pamoja na watu wengine kama familia.

Kichefuchefu
Kichefuchefu huweza kujitokeza kutokana na matibabu ya saratani kama upasuaji, dawa au mionzi. Mara nyingi kichefuchefu huisha baaada ya matibabu kumalizika. Kichefuchefu kinasababisha kutoweza kula chakula cha kutosha.
Ili kupunguza kichefuchefu yafuatayo yanaweza kusaidia:
Kujaribu vyakula ambavyo ni rahisi kuyeyushwa tumboni kama mtindi;
 Kujaribu vyakula vikavu;


Kuepuka vyakula vyenye mafuta mengi au sukari nyingi;
 Kula kiasi kidogo kidogo cha chakula taratibu na mara kwa mara;
 Kujaribu vinywaji vyenye viungo kama tangawizi, ndimu au miti;
 Kukaa sehemu yenye hewa safi na yakutosha na kuepuka harufu ya vyakula;
 Kula vyakula unavyopendelea;
 Kula vyakula vilivyopoa na baada ya kula na kujaribu kufyonza limau au ndimu;
 Kusafisha kinywa kabla na baada ya kula na kujaribu kufyonza limau au ndimu;
 Endapo kichefuchefu kinatokea wakati wa matibabu ya saratani, acha kula saa moja au mbil kabla ya matibabu kuanza, na siku ya matibabu kula vyakula visivyo na harufu kali au viungo vikali; na

Kujaribu kukumbuka wakati ambao kichefuchefu hutokea na kama inawezekana jaribu kubadili mpangilio wa kula na mshirikishe daktari.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA