Skip to main content

LISHE NA ULAJI UNAOFAA KWA WATU WENYE MAGONJWA SUGU YASIYO YA KUAMBUKIZA




Matango
4.0 MAGONJWA SUGU YASIYO YA KUAMBUKIZA

Magonjwa makuu sita yasiyo ya kuambukiza ni pamoja na: Ugonjwa wa kisukari, Magonjwa ya moyo, Shinikizo kubwa la damu, Saratani, Magonjwa ya figo na Magonjwa sugu ya njia ya hewa.

Sababu zinazopelekea kuwepo kwa magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza:

Mtindo wa maisha usiofaa unapelekea mtu kupata magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza, mtindo huu wa maisha usiofaa unahusisha mambo yafuatayo: ulaji usiofaa; kutofanya mazoezi ya mwili; matumizi ya sigara na bidhaa zitokanazo na tumbaku; matumizi ya pombe; na msongo wa mawazo.

4.1 Ugonjwa wa Kisukari

Ugonjwa wa kisukari ni hali inayotokea wakati sukari katika damu inapokuwa nyingi kupita kiwango cha kawaida kwa muda mrefu inayotokana na kongosho linaposhindwa kutengeneza kichocheo cha insulin, au insulin iliyopo katika damu kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.
Kichocheo cha insulin ndicho kinachotumika kudhibiti kiwango cha sukari katika damu. Kichocheo hiki ni muhimu sana katika kufanya sukari iweze kutumika mwilini ili kupata nishati lishe. 5



Ugonjwa wa kisukari unapompata mtu huwa ni wa kudumu, hivyo anahitaji kufuata taratibu za matibabu na maelekezo atakayopewa na mtoa huduma wa afya kwa maisha yake yote.
4.1.1 Aina za kisukari:
Kuna aina kuu mbili za kisukari ambazo ni :
Kisukari kinachotegemea insulin ( type 1 diabetes)
Kisukari kisichotegemea insulin ( type 2 diabetes)

Kuna aina nyingine ya kisukari ambayo huweza kujitokeza wakati wa ujauzito (Gestational diabetes.)
Kisukari kinachotegemea insulin:
Huwapata zaidi watoto na wenye umri chini ya miaka 35. Katika aina hii ya kisukari seli za kongosho zinazotengeneza insulin huwa zimeharibika hivyo kusababisha ukosefu au upungufu wa insulin mwilini.
Kisukari kisichotegemea insulin
Huwapata zaidi watu wenye umri kuanzia miaka 45 na kuendelea. Katika aina hii ya kisukari insulin ya kutosha inaweza ikatengenezwa katika kongosho lakini haifanyi kazi hivyo mwili kushindwa kutumia sukari kwa ufanisi.
Kisukari cha mimba
Ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi ya wanawake wakati wa ujauzito.Hali ya ujauzito husababisha ongezeko la baadhi ya vichocheo Kama Progesterone, Estrogen, na free Cortisol ambavyo huongeza kiwango cha sukari katika damu.
Wakati huohuo kichocheo cha Human Placental Lactogen huzuia insulin kufanya kazi kwa ufanisihivyo kusababisha kiwango cha insulin kuongezeka katika damu.
Mwili unaposhindwa kutengeneza insulin ya kutosha kupambana na ongezeko la sukari katika damu kisukari cha mimba hutokea. Mara nyingi hutokea mimba ikiwa na umri wa miezi mitano au zaidi na kwa kawaida huishawiki sita baada ya mwanamke kujifungua. 6
4.1.2. Viashiria hatarishi vya kupata ugonjwa wa kisukari
Kisukari kinachotegemea insulin
Kurithi katika familia, Magonjwa ya kongosho (kama saratani au uambukizo) ambayo huweza kuua seli za kichocheo kinachotengeneza insulin, kupewa maziwa mbadala (ya kopo au ya wanyama) au kumnyonyesha mtoto kwa muda mfupi, Mtoto akizaliwa na uzito mkubwa kupita kiasi, Unene au uzito mkubwa utotoni.
Kisukari kisichotegemea insulin
Uzito uliozidi au unene uliokithiri, Shinikizo kubwa la damu, Mtindo wa maisha usiofaa hususani kutofanya mazoezi, ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, na uvutaji sigara na bidhaa za tumbaku, Kuwepo kwa historia ya kisukari katika familia, Umri zaidi ya miaka 45.
Kisukari cha mimba
Kuwepo historia ya kuwa na kisukari katika familia, Kuwahi kujifungua mtoto mwenye uzito mkubwa, Mimba kuharibika mara kwa mara, Historia ya kisukari cha mimba, Mkojo kuwa na sukari mara kwa mara, Kuzaa mtoto mfu, Uzito au unene uliokithiri, Shinikizo kubwa la damu la muda mrefu, Umri zaidi ya miaka 35
4.1.3. Dalili za ugonjwa wa kisukari
Dalili za ugonjwa wa kisukari ni pamoja na:Kukojoa mara kwa mara, Kuhisi kiu sana, Kuhisi njaa sana, Kuhisi uchovu wa mwili na kukosa nguvu bila ya kufanya kazi ,Kupungua kwa uzito wa mwili na kuwa mdhaifu, Kutoona vizuri,Kuhisi kizungu zungu ,Baadhi ya viungo vya mwili kama vidole vya mikona na miguu kufa ganzi .
4.1.4. Ushauri wa ulaji Kwa mgonjwa wa kisukari
• Kula mlo kamili angalau mara tatu kwa siku, haishauriwi kukaa na njaa kwa muda mrefu.
• Kudhibiti kiasi cha nishati- lishe katika chakula, kiasi kinategemea mahitaji ya mtu binafsi.
• Kuongeza ulaji wa vyakula venye makapi mlo kwa wingi, kiasi kikubwa cha nishati lishe kitokane na vyakula venye makapi mlo kwa
7

wingi ambavyo huyeyushwa na kufyonzwa mwilini taratibu na hivyo kasi ya kuongezeka kwa sukari katika damu hupungua.
• Kupunguza kiasi cha mafuta, epuka mafuta yenye asili ya wanyama na punguza kiasi cha mafuta mengine.
• Epuka sukari na vyakula venye sukari nyingi kama vile soda, keki, biskuti, pipi, na asali, asilimia 80 ya asali ni sukari
• Epuka kunywa pombe, pia haishauriwi kunywa pombe kali kwani huleta madhara kwenye ini, usinywe pombe kabla ya kula chakula kwani huweza kusababisha damu sukatiti ( hypoglycemia
• Kula tunda katika kila mlo, ikiwezekana usimenye tunda na zingatia usalama wa chakula.
• Kula mboga mboga kwa wingi katika kila mlo, chagua mboga mboga ambazo hazina kabohaidreti kwa wingi mfano mboga za majani , nyanya matango, na saladi.
• Kupunguza uzito kama umezidi au dhibiti uzito wa mwili, ni vyema kuwa na uzito unaoshauriwa kulingana na urefu wake.
• Kupanga utaratibu wa kula chakula na matumizi ya dawa, kwa mgonjwa wa kisukari anayetumia dawa ni muhimu kupanga utaratibu maalumu wa kula na kumeza dawa ili kuzuia kupungua kwa sukari katika damu.
• Epuka kukaa kwa muda mrefu bila kula chakula. 





Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA