Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2012

JITIBU MAGONJWA 27 KWA ASALI NA MDALASINI

Mdalasini  Asali                          MDALASINI NA ASALI Taswira  ya  mtu  anayesumbuliwa  na  tatizo  la  chunusi  ambalo  linaweza  kuondoka  kwa  kutumia  mdalasini  kama  makala  haya  yanavyo  elekeza.  " MDALASINI NA ASALI vinaweza kukufanya uonekane kama picha yenye afya nzuri kama ile ya mwonyeshaji mitindo ya mavazi na muigizaji sinema Jocqol Bell." Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1 . Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wa

HABARI NJEMA KWA WANAWAKE NA WANAUME WANAUME WANAOSUMBULIWA NA TATIZO LA VITAMBI.

HABARI  NJEMA  SANA  KWA  WANAWAKE  NA  WANAUME  WANAOSUMBULIWA  NA TATIZO  LA  VITAMBI ( MATUMBO  MAKUBWA ) Utafiti  wetu  umegundua  kwamba  kuna  idadi  kubwa  sana  ya wanawake  na  wanaume  wanao  sumbuliwa  na  tatizo  la  kuwa  na matumbo  makubwa  kiasi  ama  vitambi  kwa  lugha  nyingine. Uchunguzi  wetu  umetuwezesha  kubaini  kuwa  katika  watu  kumi  wanao  tembea bararani  angalau  watatu  kati yao  wanasumbuliwa na  tatizo la kitambi. CHANZO  CHA  TATIZO  Kwa  mujibu  wa  kitabu " CHANZO, ATHARI NA TIBA ASILIA  YA  TATIZO LA  KITAMBI  NA  UNENE  KUPITA  KIASI : Orodha  Ya  Vyakula, Vinywaji na Dawa  Asilia  Zinazotibu Tatizo  la  Kitambi  Na  Unene  Kupita Kiasi , kilicho  tolewa  na  kituo  cha  utafiti  na  tiba  asilia  cha  Neema  Herbalist  cha  jijini  Dar  Es  salaam   sababu  kuu  za tatizo la  kitambi  ni  pamoja  na : 1. Ulaji  mbovu  wa  vyakula ( Ulaji usio zingatia  mlo  kamili ). Ulaji  mbovu  wa  vyakula  unajumuisha   ulaji  wa  vyakula  vya  ain

JIKINGE NA KANSA KWA VYAKULA VYA ASILI

Nyanya Kitunguu  Saumu Brokolini Beri Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  duniani, ugonjwa  wa  kansa  unatajwa  kuwa  ndio  ugonjwa  wa  hatari  zaidi  pengine  kuliko  ugonjwa  mwingine  wowote  uliowahi  kutokea  katika  historia  ya  mwanadamu.   Nchini   Tanzania  pekee  kiasi cha watu 100 hufariki dunia KILA SIKU kutokana na magonjwa ya saratani, hii  ni  kwa  mujibu  wa  taarifa  ya  Taasisi  ya  Saratani  ya  Hospitali  ya  Ocean  Road a  jijini  Dar  es  salaam  kupitia  Mkurugenzi  wake  Dk. Twalib  Ngoma. Hali i  mbaya  zaidi katika  nchi  zilizoendelea   ambako  tunataarifiwa  ya  kwamba   kuna  idadi  kubwa  sana  ya  watu  wanaopoteza  maisha  yao  kila  siku  kutokana  na  magonjwa  ya  kansa ambayo  kimsingi  yanasababishwa  na  na ulaji wa vyakula tunavyokula kila siku. Mfano  nchini  Marekani  pekee  karibu  theluthi  moja  ya  wagonjwa  wa  kansa  inasababishwa  na  vyakula  wanavyokula  kila  siku, na  hii  ni  kwa  mujibu  wa Taasisi  ya  Sarata

VYAKULA HIVI VINASABABISHA SARATANI! JIHADHARANI NAVYO!

Soseji Ugonjwa  wa  saratani  ama  kansa  unatajwa  kuwa  ndio  ugonjwa  wa  hatari  zaidi  duniani  na  unaoua   watu  wengi  zaidi  duniani.  Ugonjwa  huu  unasababishwa  na  mambo  mbalimbali  ikiwa  ni  pamoja  na  ulaji  wa  vyakula   vya aina  mbalimbali. Vifuatavyo  ni  baadhi  ya  vyakula  ambavyo  vimetajwa  katika  tafiti  mbalimbali  kuwa  visababishi  vya  ugonjwa  wa  saratani. VYAKULA VYA KUKAANGA Vyakula vingi vinavyotayarishwa kwa kukaangwa kwenye mafuta yenye moto mkali huwa na madhara kiafya na miongoni ma madhara hayo ni pamoja na kusababisha kansa ya kwenye mfuko wa uzazi. Vyakula hivyo ni pamoja na chips na vyakula vingine vinavyopikwa kwa kukaangwa kwenye mafuta. VYAKULA VYENYE CHUMVI NYINGI Vyakula vyenye chumvi nyingi vimebainika navyo kusababisha kansa. Vile vile inaelezwa kuwa chumvi huwa kama chakula kwa bakteria wa kansa tumboni. Kansa ya tumbo inadaiwa kuua watu wengi nchini Japan kutokana na jamii hiyo kupenda sana vyakula vyenye chumv